Waziri mkuu mh Kassim Majaliwa |
Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania
Mh.Kassimu Majaliwa amewasimamisha kazi maafisa watatu wa Serikali wilayani
Chato kwa makosa tofauti ikiwemo ya ubadhilifu wa fedha ,na madai ya fedha kwa
sakosi mbili ambazo alikuwa akidaiwa Afisa ushirika ikiwa ni pamoja na kuuwa
ushirika wa sakosi ya umoja.
Waliosimamishwa ni mhandisi wa maji Peter
Ngolemo kwa tuhuma za kupotea kwa pampu katika kijiji cha Karebezo Kata ya
Mirembe, Warioba Mwita ambae ni Afisa Ishirika kwa kile kinachodaiwa kuwa
alikopa fedha katika sakosi na kushindwa kurejesha fedha hali iliyopelekea
kuwepo kwa migogoro katika sakosi mbili ya walimu na umoja,na Afisa maendeleo
ya jamii pamoja na Dionizi Mulayoba kosa lake ni ubatilifu wa fedha.
Aidha waziri Majaliwa amewataka watumishi wa
serikali kubadilika na kuhakikisha wanafuata misingi ya uadilifu pindi wawapo
kazini ikiwa ni pamoja na kuwa wawajibikaji katika maeneo ambayo wanatakiwa
kujituma kwa bidii zaidi ili kuleta maendeleo kwa nchi na kwamba hakuna mtu
yeyote atakaye lindwa endapo akienda kinyume na kanuni na sheria ya nchi katika
swala la uwajibikaji.
Waziri mkuu leo anatarajia kumaliza ziara yake
ya kikazi mkoani hapa kwa kukutana na viongozi wa ngazi mbali mbali ikiwa ni
pamoja na kuzungumza na wananchi wa Katoro wilayani Geita.
No comments:
Post a Comment