Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2016-04-15

BANANA ASEMA ANAFANYA MUZIKI KAZI, SIO KUTAFUTA SIFA

Akizungumza na Bongo5 Jumatano hii, Banana amesema baadhi ya wasanii wanaofanya vizuri zaidi yake huwa wanatumia ‘kiki’ kitu ambacho yeye hakihitaji.

“Mimi nafanya muziki kazi, siyo kutafuta sifa,” alisema Banana. “Kuna wasanii wengi wamefika mbali licha ya wachache ambao wamefika mbali kutokana na juhudi zao, Lakini baadhi yao wanaishi maisha ya ‘kiki’, anajulikana kweli na nyimbo zinapigwa mbali lakini sometime inafika hatua hata kodi ya nyumba nakosa,”

“Vitu ambavyo mtu anazungumza kwenye interview ni tofauti na maisha yake, mtu hata gari la kutembelea hana alafu anasema amefika mbali. Lakini hizo pia ni itikadi ambazo zilifanywa na kaka zetu pamoja na dada zetu. Sasa hivi game imekuwa kwa maana siyo lazima tu ujue kuimba tu ndiyo ufanye vizuri hata ukiwa na mipango fulani unaweza kwenda mbali zaidi,” aliongeza.

Banana alisema hana haraka kwenye muziki, na anajipanga kufanya muziki mzuri ambao unawapendeza mashibiki wake wa kila siku.

No comments:

Post a Comment

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina