Akizungumza katika hafla ya kuwaaga wagonjwa wenye tatizo la midomo sungura Kaimu mkurugenzi wa mgodi wa dhahabu wa Geita, Habati Cawoodi amesema kuwa mgodi huo umefurahishwa na zoezi hilo, ambalo walilianza mwaka 2004 na kwamba jumla ya watu elfu 1,200 wamekwisha kufanyiwa upasuaji na wakarudi katika hali yao ya kawaida.
Akimwakilisha mkuu wa wilaya, Kaimu katibu mkuu wa wilaya ya Geita Saashisha Magwe,ameeleza kuwa ni vyema kwa wananchi wenye matatizo ya midomo sungura kujitokeza na kutokuendelea kukaa na ugonjwa huo kwani unatibika.
Meneja wa mawasiliano na mahusiano mgodi wa GGM, tenga bintenga, amesema furaha ya mgodi ni kuona namna watu wanaporejea wanakuwa wako katika hali nzuri na yenye furaha.
Aidha kwa upande wao wananchi na wazazi wa watoto wenye matatizo hayo wameushukuru mgodi wa ggm namna ambavyo umeendelea kuwajali wananchi na kutoa huduma za afya ambazo ni za bure.
No comments:
Post a Comment