Ajali ya moto imetokea katika mtaa wa Balenge kata ya Kalangalala katika nyumba ya kulala wageni majira ya leo mchana wilayani na mkoani Geita na kusababisha uharibifu wa vitu vya thamani baada ya nyumba kuungua moto.
Wakizungumza na storm habari wakazi wa eneo hilo ambao wamejitokeza eneo la tukio kushuhudia huku wakisaidia zoezi la uokoaji wamesema kuwa moto huo ulianzia katika chumba baada ya mtumiaji wa chumba hicho kuacha jagi la kuchemshia maji likiwa halijazimwa kwenye umeme.
Akizungumza katika eneo la tukio kaimu kamanda wa jeshi la zimamoto na uokoaji mkoani Geita Inspector Christina Sunga amewataka wananchi wa mkoani hapa kwa ujumla kuwasiliana na jeshi hilo haraka pindi zinapotokea ajali kama hizo kwa kupiga simu moja kwa moja jeshi la zimamoto ili kupatiwa msaada.
Kwa upande wake Evarist Mwanakatwe ambaye ni Afisa wa kitengo cha dharula katika mgodi wa dhahabu wa Geita (GGM) baada ya kufika katika eneo la tukio wakiwa na gari la zimamoto na kuwezesha zoezi la uokoaji kumalizika katika hali ya usalama amewapongeza wakazi wa mtaa wa Balenge kwa kuchukua uamuzi wa kutoa msaada wa uokoaji.
Naye mtoto wa mmiliki wa nyumba hiyo Bainika Kwitega Balenge ameshukuru wananchi pamoja na jeshi la zimamoto wakisaidiana na mgodi wa GGM kwa kuwezesha uokoaji wa nyumba hiyo.
No comments:
Post a Comment