Mwenyekiti wa Kitongoji cha Bweya katika
Kijiji cha Bweya mkoani Geita, Augustine Katemi (42) ameuawa baada ya
kufumaniwa akifanya mapenzi na mke wa mtu vichakani.
Mwenyekiti huyo alifariki dunia papohapo
baada ya kudaiwa kushambuliwa kwa sime na mume wa mwanamke huyo, mkazi wa
Kijiji cha Luchili, Wilaya ya Buchosa mkoani Mwanza.
Tukio hilo lilitokea saa nne usiku Machi
28 baada ya marehemu kudaiwa kukutwa akifanya tendo la ndoa na Chausiku
Isangula (32).
Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu tukio
hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Latson Mpojoli alisema hana za
taarifa za tukio hilo na kuahidi kufuatilia.
Ilielezwa kuwa Katemi aliuawa baada ya
kushambuliwa kwa sime na kufa papohapo na baada ya tukio hilo, mtuhumiwa
anadaiwa kumshambulia mkewe kwa kutumia sime hiyohiyo na kumsababishia majeraha
makubwa sehemu mbalimbali za mwili na amelazwa kwenye Kituo cha Afya cha Nzera.
Mtendaji wa Serikali ya Kijiji cha
Bweya, Samson Walwa alisema baada ya kutokea tukio hilo wananchi waliendesha
msako na kumtia mbaroni mtuhumiwa wakati akijaribu kutoroka kuelekea Sengerema.
Walwa alisema mtuhumiwa alikamatwa
nyumbani kwa Edward Iswalala alipokuwa amefikia kwa siri kutoka Luchili ili
kufuatilia mwenendo wa mkewe ambaye anadaiwa kuwa awali alimuaga kuwa anakwenda
kumsalimia baba yake mzazi anayetibiwa kwa mganga wa kienyeji.
“Inavyosemekana alikuwa akifuatilia
mienendo ya mke wake… sisi tulipomkamata tumemkabidhi Kituo cha Polisi cha
Nzera pamoja na nguo za marehemu (mwenyekiti) na zile za mkewe kwani alipofanya
mauaji hayo alizichukua nguzo zao hadi tulipomkata nazo,” alisema Walwa.
Mmoja wa wananchi walioshuhudia tukio
hilo, Jumanne Tole alisema, Chausiku alimuaga mumewe kuwa alikuwa anakwenda
kijiji cha Kalebezo kumsalimia baba yake mzazi kwa waganga wa tiba asilia
alikokuwa anatibiwa lakini baada ya kufika na kumsalimia, alikwenda kwa kaka
yake aitwaye Ndagabwene Isangula huko Bweya alikofikwa na mkasa huo.
No comments:
Post a Comment