Kamishina msaidizi wajeshi la polisi mkoani Geita, Mponjoli Lotson.
Jeshi la polisi mkoani Geita limejipanga kuimarisha ulinzi na usalama katika sikukuu ya pasaka itakayoadhimishwa jumapili march 27 duniani kote ili kuwawezesha wananchi kusherehekea kwa amani na utulivu siku hiyo.
Akizungumza na storm habari ofisini kwakwe kamishina msaidizi wa jeshi la polisi mkoani hapa, Mponjoli Lotson amesema kuwa uamuzi huo umekuja baada ya kugundua kuwa baadhi ya watu wamekuwa wakitumia mwanya huo kufanya uhalifu kutokana na kuwepo kwa muingiliano mkubwa wa wananchi katika sehemu mbalimbali.
Aidha kamanda Mponjoli amebainisha kuwa maeneo yote wameimarisha ulinzi ikiwemo kumbi za starehe, makanisa, sehemu zote za njia kuu, huku askari wakipangwa kila mitaa.
Aidha kamanda amewataka wananchi kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi kwa kutoa taarifa sehemu husika pindi wanapokuwa na na mtu ama kikundi cha watu.
No comments:
Post a Comment