RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza
la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amemuapisha Bwana Said Hassan Said,
kuwa Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyeikiti wa Baraza la Mapinduzi alimteua Bwana Said Hassan jana kushika wadhifa huo kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Kifungu cha 55 (1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.
Hafla ya kumuapisha Mwanasheria Mkuu
huyo ilifanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Miongoni mwao ni Jaji Mkuu wa Zanzibar
Mhe. Omar Othman Makungu, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi
Dk. Abdulhamid Yahya Mzee, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi
Khamis.
Wengine ni Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar
Sheikh Hassan Othman Ngwali, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmoud Mussa
Wadi, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib,Washauri wa
Rais wa Zanzibar na viongozi wengine wa Serikali.
Viongozi mbali mbali na watendaji
waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Said Hassan Said kuwa Mwanasheria Mkuu
wa Zanzibar katika ukumbi wa mikutano Ikulu Mjini Zanzibar leo asubuhi.
No comments:
Post a Comment