Wadau mbalimbali mkoani Geita wametakiwa kuwasaidia watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu na sio kuiachia serikali pekee.
Hayo yamesemwa na diwani wa kata ya Buhalahala Musa Kabese wakati alipokuwa akikabidhi sare za shule kwa wanafunzi waishio katika mazingira magumu katika shule za msingi Mwatulole,, Nguzo mbili,, na Buhalahala ikiwa ni moja ya ahadi zake alizoahidi kipindi cha kampeni.
Akitoa shukrani kwa niaba ya walimu,, mwl mkuu wa shule ya msingi Mwatulole Catherini Mgusi amesema kuwa msaada huo utawasaidia watoto kujumuika na wenzao vizuri kwani hapo awali walikuwa wakivaa sare zilizochakaa na kuonyesha baadhi ya sehemu za miili yao kitendo kilichowafanya watoto hao kujisikia aibu.
kwa upande wake mwenyeki wa shule hizo Lucas Kidengana amewaomba wafadhili kuisaidia shule hiyo ili waweze kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili shule hiyo .
Aidha kwa upande wa wanafunzi wa shule hizo wametoa shukrani zao baada ya kupokea msaada huo ambapo wamemuomba diwani Kabese kusaidia kutatua na matatizo mengine yanayokabili shule hizo.
No comments:
Post a Comment