Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2016-08-20

Kigwangala aagiza kufungwa kwa vituo vya afya visivyokuwa na huduma ya upasuaji mkoani Geita ndani ya miezi sita

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk Hamis Kigwangalla amemwagiza mkuu wa mkoa wa Geita meja jenerali Ezekiel Kyunga kuhakikisha vituo vyote vilivyopewa hadhi ya vituo vya afya mkoani hapa vinatoa huduma ya upasuaji ili kuendelea kupunguza vifo vya akina mama na watoto.

 

Dkt Kigwangala ameyasema hayo mapema hii leo alipofanya ziara ya siku moja mkoani hapa ya kutembelea hospitali ya rufaa ya mkoa pamoja na vituo 2 vya afya ambavyo ni kituo cha Nyankumbu na hospitali ya Makoye kwa lengo la kukagua utendaji kazi katika sekta ya afya.

 

Amesema kuwa ni vyema sasa vituo vyote vilivyopewa hadhi ya kuitwa vituo vya afya vikawa na huduma za upasuaji  huku  akisisitiza kuwashusha hadhi waganga wa vituo na vituo vyao vitakavyoshindwa kutoa huduma hiyo hadi katka ngazi ya zahanati.

 

Akisoma taarifa ya utekelezaji mbele ya naibu waziri mganga mkuu wa mkoa wa Geita dkt Kisala Joseph amesema kuwa serikali inaendelea na ujenzi wa vituo 2 vya afya mkoani hapa vitakavyokuwa vikitoa huduma ya upasuaji ambavyo vitajengwa katika wilaya ya Mbonge na Chato,


Naibu waziri akiwasili mkoani Geita
Naibu waziri akitoa maagizo kwa watumishi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Geita

 

No comments:

Post a Comment

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina