2016-09-16
LIPULI FC YAITISHA AFRICAN SPORTS
Akizungumza juu ya hatima hiyo,Mratibu wa Mazoezi na pia ni Msimamizi wa Usajili,Haruna Saleh,amesema kuwa wamejianda kuanza vizuri msimu huu katika Ligi hiyo kwani wamefanya maandalizi ya kutosha na kambi yao waliifanyia Dar es salaam katika uwanja wa Karume wakiwa chini ya Kocha Mkuu Richard Amache anayekinoa kikosi hicho.
“Kilichobaki ni kuwaomba mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanjani kwa kuja kuwapa hamasa ya ushindi wachezaji wao ili waweze kufanya vizuri na hatimaye kuipandisha Ligi Kuu msimu ujao kwani wanaamini ligi itakuwa ngumu kwa kila timu kutaka kupanda Ligi”alisema Saleh
Lipuli wataanza kampeni yao ya kutaka kupanda Ligi kwa kuwakaribisha Wana kimanumanu ambao msimu uliopita waliweza kushuka daraja kutokana kuwa na migogoro ya Uongozi na kupelekea timu tatu za Tanga kuweka rekodi Dunia kwa kushuka kwa pamoja ambazo zilikuwa ni African Sports,JKT Mgambo na Coastal Union.
About CHOMBONI MEDIA
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment