Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2016-09-05

SANGOMA ATUPWA JERA MIAKA MITATU KWA KUMTAPELI MLEMAVU KUMTENGENEZEA FEDHA ZA MAJINI ILI ATAJIRIKE.



MAHAKAMA ya Mwanzo ya Masumbwe Wilayani Mbogwe  imemuhukumu  kifungo  jera miezi 36  na kuchapwa viboko 24 matakoni  Mganga wa Jadi (Sangoma ) Sabas Majaliwa (42)mfipa mkazi wa Mwanza  baada ya kumtapeli mlemavu wa miguu Paul Mpangabule  kwamba atamtengenezea fedha za utajiri kwa njia ya majini .


Hakimu wa mahakama  hiyo ya mwanzo masumbwe mh Sunga  Emmanuel Mechara amesema  kifungu cha 32 cha kanuni za mwenendo wa mashauri ya jinai katika mahakama za mwanzo ambayo ni nyongeza  ya tatu ya Sheria ya mahakama za mahakimu sura ya 11 iliyofanyiwa mapitio 2002.
amemuhukumu Sabas Majaliwa kwa kosa la kujipatia Fedha kwa njia ya udanganyifu kinyume na kifungu cha 302 sura ya 16 kanuni ya adhabu.

Mh Mechara amesema Sabas Majaliwa ametiwa hatiani baada ya kukiri shitaka aliloshtakiwa nalo na amepewa adhabu ya kifungo jera miaka 3 sawa na mizi 36 pamoja na kuchapwa viboko 24 matakoni baada ya kupimwa na daktari ili iwe fundisho kwa waganga wengine wa jadi wanaendesha mchezo huo wa utaperi wa kuwatengenezea fedha za majini ili watajirike.

Mahakamani hapo ilidaiwa kuwa majaliwa siku ya agosti 20 mwaka huu alimtapeli sh. 435,000 Paul Mpangabule 53 mlemavu wa miguu yaani kiwete mkazi wa mtaa wa shy A nyakafuru  akiwa yeye na mke wake watengenezewe fedha za utajiri za majini,ili watajirike.

Mganga huyo baada ya kuchukuwa fedha sh 435,000 alifika na  vitambaa viwili cheupe na chekundu chungu kidogo ,udi na ubani   na sanduku kubwa litakalojazwa fedha   na chupa aliyodai inamafuta ya Binadamu  ambayo yalipakwa kwenye fedha hizo wakainamishwa kwenye sanduku  na kuogeshwa  fedha baada ya hapo mganga akatoweka na fedha hizo akidai anazipeleka makaburini kufanya tambiko .

Aliporudi mganga akawaomba sh. Milioni tatu ili wazichanganye na fedha za majini     watakatishe fedha hizo na zile za jasho lao wakakosa akawaambia wakakope ili wazilete waanze kuhesabu ndipo walipopata ufahamu na hatimaye askari polisi kituo cha masumbwe wakamkamata na kumfikisha mahakamani.


Mshitakiwa majaliwa ameomba apunguziwe  adhabu kwa kuwa ana mke ,watoto na mama yake mjane anaowatunza na wanamtegemea.

No comments:

Post a Comment

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina