Viongozi wa CCM kata ya Nyankumbu wote wamejiuzulu nyadhifa zao kwa wakati mmoja kwa madai ya kuwa Viongozi wa Wilaya wameshindwa kumsaidia katibu wa tawi la Nyantorotoro A Kazungu Meliki aliyemwagiwa tindikali Agusti 31.
Wamesema tangu kutokea kwa tukio hilo hakuna kiongozi hata mmoja aliyekuja japo kumjulia hali ambapo kwa sasa hali ya Kazungu kiafya inazidi kuwa mbaya huku watendaji katika kata wakiendelea kutishiwa maisha yao lakini Chama hakiwajali na hawako tayari kuona wengine wakiumizwa au kupoteza maisha.
No comments:
Post a Comment