Jeshi la polisi wilayani Bukombe mkoani geita limemfikisha mahamani mwalimu Jackson Jilaa wa shule ya msingi kakoyoyo kata ya Bulega kwa kosa la kubaka na kumsababishia ujauzito mwanafunzi wake mwenye umri wa miaka 16 aliyefaulu kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu katika shule ya sekondari Bulega.
Mbele ya hakimu mkazi mfawidhi mwandamizi wa mahakama ya wilayani hapo Gabriel Kulwijira, mwendesha mashitaka wa polisi mkaguzi msaidizi Neema Naruke ameieleza mahakama hiyo kuwa mshitakiwa bila aibu na bila kujali maadili ya utumishi alimbaka mwanafunzi wake na kumsababishia ujauzito.
Amesema kuwa kitendo alichokifanya Mwalimu Jackson Jilaa cha kumharibia maisha mwanafunzi wake ambae alifaulu mtihani wa darasa la 7 ni kitendo cha udhalilishaji na pia ni ukatili wa kijinsia.
Hata hivyo mshtakiwa mwalimu Jackson amekana shitaka na hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya Gabriel Kurwijila amemrudisha rumande hadi hapo kesi itakapotajwa tena.
No comments:
Post a Comment