Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Ndg Henry J. Semwanza
Waziri
wa kilimo Mhe Dkt Charles Tizeba amemuagiza Katibu mkuu wa Wizara ya
Kilimo Mhandisi Methew Mtigumwe kumsimamisha kazi mara moja Mkurugenzi
Mkuu wa Bodi ya Sukari Tanzania Ndg Henry J. Semwanza kuanzia leo
Novemba 9, 2017.
Kwa
agizo hilo lililotolewa na Waziri wa Kilimo Dkt Tizeba, Mkurugenzi huyo
atatakiwa kurejea kwa mwajiri wake ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya
Kilimo kwa ajili ya kupangiwa kazi nyingine.
Simwanza anasimamishwa kazi kutokana na mwenendo wake wa utendaji akiwa Msimamizi Mkuu wa Bodi ya Sukari kutoridhisha.
Simwanza amehudumu katika nafasi hiyo akiwa Mkurugenzi wa Bodi ya Sukari tangu mwaka 2011.
No comments:
Post a Comment