Bw.
Jeremiah Ragita aliyejifanya kuwa Wakili akitokea Kampuni ya Sheria ya
Faithful Attorney Advocates kwa mujibu wa Naibu Msajili, Mahakama ya
Ardhi, Mhe. Frank Mahimbali anasema Wakili huyo feki alikamatwa mapema
Novemba 08 katika Mahakama hiyo akimsimamia Mleta maombi Nunu Mhusin
Mkwata.
******
Mhe.
Mahimbali anasema kuwa upande wa pili ambao unasimamiwa na Wakili Maros
Gabriel kutoka Kampuni ya Sheria ya ‘Common Law Chambers’ ulimtilia
shaka Bw. Jeremiah Ragita kama kweli ni Wakili ndipo alipofanya upekuzi
kwenye Ofisi ya TLS na kuambiwa kuwa hawana jina hilo.
Hata
hivyo Mhe. Mahimbali alienda mbali na kumuandikia barua Msajili wa
Mahakama Kuu (RHC) na kujibiwa kuwa hakuna Wakili aliyesajiliwa kwa jina
hilo.
Kwa
mujibu wa Naibu Msajili kesi hiyo ilipoitwa mbele ya Mhe. Jaji
Crencesia Makuru, Wakili Maros alimueleza Mhe. Jaji kuwa mwenzake wa
upande wa pili sio Wakili na kisha akatoa vielelezo kutoka katika Ofisi
ya Msajili Mahakama Kuu na Ofisi ya TLS ndipo Bw. Ragita akakiri kuwa
yeye si Wakili.
Hata
hivyo Bw. Ragita alikamatwa na kupelekwa Polisi Kituo cha Kati (Central
Police) jijini Dar es Salaam kwa ajili ya hatua stahiki za kisheria.
Mahakama
inapinga vikali vitendo vya ulaghai (Mawakili feki, vishoka)
vinavyofanywa na baadhi ya Wananchi kwa lengo la kujipatia kipato.
(Imetolewa na Kitengo cha Habari, Elimu na Mawasiliano, Mahakama).
No comments:
Post a Comment