Serikali wilayani Chato mkoani Geita imeahidi
kuvitaifisha vyombo vyote vya moto vitakavyokamatwa vikisafirisha samaki
wachanga kutoka ziwani kwenda maeneo mengine ndani na nje ya wilaya hiyo.
Kauli hiyo imetolewa
na mkuu wa wilaya ya Chato Bw Shabani Ntarambe wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juu ya uvuvi
haramu mbapo amesema kuwa wamejipanga kuhakikisha wanakagua magari na pikipiki kwa
lengo la kuwabaini baadhi ya watu wanaosafirisha samaki wachanga kinyume na
sheria.
Amesema hatua hiyo
imekuja mara baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema juu ya uwepo wa
madereva bodaboda na magari ya abiria wanaotumia vyombo hivyo
kutorosha samaki wachanga jambo ambalo halikubariki.
Nae mwenyekiti wa
uhifadhi wa rasilimali za uvuvi BMU wilayani humo Bw Bashiri Manampa
amesema kuwa amejipanga
kuanzisha msako mkali kwa kushirikiana na maofisa wa uvuvi wilayani humo kwa
lengo la kuendelea kupambana na wavuvi haramu katika ziwa victoria.
No comments:
Post a Comment