Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2018-03-23

WAKAMATWA WAKIJIFANYA USALAMA WA TAIFA: DODOMA

 

Jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma linawashikilia watu 14 kwa makosa mbalimbali wakiwemo wanne kati yao kwa kujifanya maafisa wa jeshi la wananchi wa Tanzania JWTZ na usalama wa Taifa huku wakitumia nyadhifa hizo kujipatia mali kwa njia za udanganyifu.


Kamanda wa jeshi la polisi Mkoa wa Dodoma Gilles Mroto akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake amewataja waliokamatwa katika tukio hilo kuwa ni Shaban Ramadhan Kwiyela (58) mkazi wa Igunga Tabora, Emmanuel Kasunga ( 45) mkazi wa Mtera Iringa, Juma Almasi Pembambili (33) mkazi wa Sai jijini Mbeya pamoja na Emmanuel Hassan Mwangolela (50) mkazi wa mtaa wa Ghana jijini Mbeya.
 
Katika tukio la pili wamekamatwa watu wawili kwa kujihusisha na wizi wa pikipiki huku wakitumia mbinu ya kuiba pikipiki kutoka Dodoma na kwenda kuziuza Kiteto Manyara na zingine wakiiba kutoka Kiteto na kuzileta kuziuza hapa Mkoani Dodoma.

Kamanda mroto amesema tukio la tatu wamemkamata kijana Abdalah Hamza Salum (20) dreva wa bodaboda mkazi wa Area A Dodoma kwa kosa la unyang’anyi ambapo hutumia pikipiki yake yenye namba za usajiliu MC. 366 BJR aina ya boxer kukwapua mikoba ya wapita njia na akipakia abiria huwapeleka katika maficho na kuwatishia sime kisha kuwapora vitu mbalimbali zikiwemo simu za mkononi, mikufu na vito vya thamani.

Katika tukio la mwisho kamanda Mroto amesema wanawashikilia watu 6 akiwemo raia wa china kwa kosa la kuchezesha mchezo wa kamali bila kibali maalumu katika mkoa wa dodoma na hivyo kuikosesha serikali mapato na katika matukio yote kamanda mroto amesema mkoa wa dodoma utaendelea na kila aina ya uhalifu utakaojitokeza katika mkoa wa Dodoma

1 comment:

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina