Rais Mteule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dkt. Ali
Mohamed Shein ameapa kuwa Rais kwa mujibu wa katiba katika kuongoza wananchi wa
Zanzibar kwa muda wa miaka 5.
Rais Mteule ameapishwa na Jaji Mkuu wa Zanzibar Jaji Omary
Othman Makungu mbele ya viongozi wa nchi pamoja na viongozi wa dini na
kushuhudiwa na mamia ya wananchi katika uwanja wa Amani mjini Unguja.
Baada ya Rais Shein kuapishwa viongozi wa dini wameomba dua
wakiongozwa na Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji Khamis na kufuatiwa na
Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Zanzibar Mhashamu Augustino Shayo na
Askofu wa Anglikana Dayosisi ya Zanzibar Padre Michael Henry Hafidh.
Viongozi mbalimbali wamehudhuria Kiapo hicho akiwemo Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mama
Samia Suluhu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, viongozi wastaafu wa kitaifa na
mamia ya wananchi.
Aidha Rais Dkt. Ali Mohamed
Shein ameapishwa na kuwa Rais wa awamu ya saba kwa serikali ya mapinduzi ya
Zanzibar na kukagua gwaride rasmi, pamoja na itifaki nyingine kufuatia
No comments:
Post a Comment