Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2016-03-21

GEITA GOLD YANUKIA KUPANDISHWA LIGI KUU-2016/2017.

Kikosi cha Geita Gold

Klabu ya wachimba Migodi wa Geita inakaribia kupandishwa kucheza ligi kuu soka Tanzania bara baada subira ya muda mrefu ya kuamua sakata la upangaji wa matokeo katika michezo miwili ya mwisho ya ligi daraja la kwanza ambayo matokeo yake yameonekana kugubikwa na utata mkubwa.

Geita iliibuka na ushindi wa mabao 8-0 dhidi ya Kanembwa JKT,huku Polisi Tabora wao wakichomoza na ushindi wa mabao 7-0 dhidi ya maafande wa Jkt Oljoro,matokeo yaliyoibua hisia tofauti kutoka kwa wafuatilia wa michezo hiyo,kiasi cha kulishtua shirikishao la soka nchini Tff ambalo nalo likalazimika kuzuia kutangazwa kwa timu iliyopanda daraja kuingia ligi kuu msimu ujao kutokana na utata huo.
Tarifa za chini chini zilizotufikia  zinasema kuwa kwa hali ilivyo upo uwezekano wa asilimia 90% kwa timu ya Geita Gold kupandishwa kuingia ligi kuu.




Rais wa Tff Jamal Malinzi alijitokeza hadharani kupitia akaunti yake ya Tweeter akisema kuwa wameamua kuzuia kutangazwa kwa matokeo mpaka kamati ya nidhamu ikae na kulijadili suala hilo.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati hiyo ya nidhamu ya shirikisho la mpira Tff,Abbas Talimba,alipozungumza amesema kikao cha kwanza cha kujadili sakata hilo kimefanyika jana (jumapili) lakini kimeshindwa kuibuka na maamuzi kutokana na mmoja wa watu wanaotakiwa kuwemo kwenye kikao hicho kutofika.
“tumeshindwa kufikia maamuzi kutokana na kukosekana kwa kiongozi wa chama cha soka kigoma,kwahiyo kikao kitaendelea tena siku ya alhamis na tungependa jambo hili liwe limemalizika siku hiyo” Amesema Talimba.
Hata hivyo alipoulizwa kama miongozi mwa watu wanaotajwa kuwemo katika sakata hilo la upangaji wa matokeo wamo pia viongozi wa Tff?,Talimba amesema hakuna kiongozi yeyote wa shirikisho aliyetajwa, isipokuwa wale waliotajwa ni viongozi kutoka vyama vya mikoa.



No comments:

Post a Comment

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina