Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2016-03-21

MAYANJA AJIVUA KWA BANDA,ASEMA “SIKUBALI KUPANDWA KICHWANI NA MCHEZAJI”


Abdi Banda.
Siku chache tu baada ya uongozi wa Simba kumsimamisha kwa kipindi cha mwezi mmoja mlinzi Hasan Isihaka kutokana na kile kinachoelezwa kuwa ni utovu wa nidhamu,Kocha mkuu wa Simba Jackson Mayanja ameibuka na kumtolea uvivu mlinzi mwingine Abdi Banda kutokana na kitendo kama hicho cha utovu wa nidhamu.

Kwa mujibu wa Mayanja,Abdi Banda alionesha utovu wa nidhamu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coast Union uliopigwa siku ya jumamosi kwenye uwanja wa mkwakwani mjini Tanga,alipomsimamisha mchezaji huyo kutoka benchi na kumwambia apige jaramba tayari kwa kuingia uwanjani kuongeza nguvu.
Kwa sababu anazozijua mwenyewe,Banda aligomea agizo hilo la kocha wake akidai kwanini asianze tangu mwanzo wa mchezo na badala yake anaanzia benchi,kitendo alichokitafsiri kama kutoaminiwa na kocha wake.
Abdi Banda ni mtoto wa beki wa zamani wa Simba Hassan Abdi Banda,anayetajwa kuwa alikuwa na nidhamu ya hali ya juu miongoni mwa wachezaji wenzake pamoja na benchi la ufundi kwa ujumla.
“Mimi kama kocha wa Simba naweza kumpangia mchezaji chochote cha kufanya kwa kuwa kazi iliyomleta kikosini ni kucheza mpira,sasa nashangaa anakataa agizo langu?tena mbele ya watazamaji!,hivi mimi na yeye nani yupo juu ya mwenzake?
Nasema hivi mchezaji amesaini mkataba wa kufanya kazi ya kucheza mpira kwenye klabu na kama hataki kutimiza wajibu wake kwangu hana nafasi hata kidogo,mimi siwezi kumbembeleza wakati anajua wajibu wake.Amesema Kocha Jackson Mayanja.

Banda akichuana na Donald Ngoma
Mayanja ameongeza kuwa anamshangaa Banda kumgomea maelekezo yake,wakati wachezaji wengine wote wanayo nidhamu na wanamsikiliza kila anachowaelekeza.
Hata hivyo alipoulizwa kama adhabu gani atakayompa Banda kutokana na kitendo hicho,Mayanja amesema kamati ya nidhamu ya Simba ndiyo yenye jukumu la kuamua adhabu gani anayostahili kwa kile alichokifanya.
Huyo ni mchezaji wa pili kwa hivi karibuni kuripotiwa kuonesha utovu wa nidhamu ndani ya klabu ya Simba,akitanguliwa na Hassan Isihaka ambaye anatumikia adhabu ya kutocheza kwa kipindi cha mwezi mmoja.


No comments:

Post a Comment

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina