Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina

Search This Blog

Breaking

Serikali kuja na mpango wa kodi ya nyumba kulipwa mwezi mmoja mmoja

TANGAZA NASI HAPA


2016-09-10

MTENDAJI ATUHUMIWA KWA UBADHIRIFU WA FEDHA ZA KIJIJI CHA BUJULA.



Hapa Mkuu wa wilaya akimsikiliza kijana ambae ni mlemavu wa viungo katika kijiji cha Bujula.
Mkuu Wa Wilaya Ya Geita,Herman Kapufi,Amemwagiza Mkurugenzi Wa Halmashauri Ya Wilaya Ya Geita,Kuhakikisha Anamwamisha Mtendaji Wa Kijiji Cha Bujula Sekile Mhagwa  Kuanzia Leo Ni Kutokana Na  Kuwa Na Tuhuma Za Kutumia Fedha Kiasi Cha Sh,Million 9, Kinyume Na Matumizi Ya Fedha Hizo ,Ambapo Katika Fedha Hizo Kulikuwa Na Fedha Za Watoto Waishio Mazingira Magumu,Na zingine Za Watu Ambao Wameathirika Na
VVU Na Pesa Nyingine Ya Mfuko Wa Jimbo.


Hatua Hiyo Imekuja Baada Ya Mkuu Wa Wilaya Kufanya Ziara Ya Kikazi Yenye Lengo La Kuzungumza Na Wananchi Na Kutatua Changamoto Ambazo Zimekuwa Zikiwakumba Wananchi Wa Wilaya Ya Geita.

Akiwa Katika Mkutano Na Wananchi Kata Ya Bujula,Diwani Wa Kata Hiyo Amina Kanijo,Amefikisha Malalamiko Yake Mbele Ya Mkuu Wa Wilaya Akimtuhumu Mtendaji Wa Kata Kutumia Fedha Kinyume Na Utaratibu hali ambayo imesababisha baadhi ya maendeleo ya Kata hiyo kusimama.


Kutokana Na Malalamiko Hayo Ilimlazimu Mkuu Wa Wilaya Ya Geita,Kutoa Maagizo Ya Kuhakikisha Mwalimu Ambae Ametuhumiwa Na Matumizi Ya Fedha Kukamatwa Lakini Pia Mkurugenzi kumwamisha mtendaji aliyetumia fedha kinyume na taratibu zilizowekwa .
"Mtendaji kama ameshalipa fedha hafai kuendelea  kubaki katika kituo hiki kuanzia jumatano mkurugenzi leta mtendaji mwingine mchapa kazi ambae anaweza kuwafanyia kazi wakazi wa bujula"alisema Kapufi.


Kapufi,Amewaagiza Watumishi Wote  kuwa Na Maadili Katika Kuwatumikia Wananchi Na Kuachana Na Tabia Ya Kuwa Kero Katika Jamii Wanazoziongoza.


Burudani ni sehemu ya maisha ya mwanadamu hapa mkuu wa wilaya akionesha umahiri wake wa kupiga Ngoma.

Mkuu wa wilaya Geita,Herman Kapufi akitoa maagizo kwa wananchi wa kijiji cha Bujula .
Unapo fanya kazi nzuri unaitaji kupongezwa hapa akikipongeza kikundi cha ngoma cha kijiji cha Bujula.


Mwenyekiti wa kijiji cha Bujula ,Hamis John akifungua Mkutano.


Diwani wa kata ya Bujula,Amina Kanijo,akielezea matatizo yaliyopo kijijini hapo mbele ya mkuu wa wilaya.


Mkuu wa wilaya ya Geita,Herman Kapufi akiwasisitiza watendaji kuwa waadirifu.

Sekile Mhagwa Mtendaji wa Bujula aliyetakiwa kupatiwa uhamisho kutokana na ubadirifu wa fedha akiwa katika pozi.

Mwenyekiti wa kijiji cha mduhani,Mashauri Kifaru akitoa ufafanuzi kwa wananchi.


Wananchi wakielezea matatizo yao.

Wakina mama pia hawakubaki nyuma kutoa yao ya moyoni.

Mkuu wa wilaya na watendaji wa kijiji na kata wakikagua kisima kilicholalamikiwa na wananchi wa Bujula.




No comments:

Post a Comment

Tunakupa habari motomoto na uchambuzi wa kina